WANA-POLO waiomba Serikali kuingilia kati vitendo vya unyanyasaji na uzalilishaji dhidi yao.

In Kitaifa
Wakazi wa mji mdogo wa Merelani wameiomba serikali kuingilia kati vitendo vya unyanyasaji na uzalilishaji vinavyoendelea dhidi ya wafanyakazi katika migodi ya wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite maarufu kama WANA-APOLO , baada ya Mfanyakazi kutoka moja ya migodi hiyo kunusurika kufa baada ya kujeruhiwa vibaya kwa kuchomwa moto na mwajiri wake.
Wakazi hao wakiongozwa na Diwani wa kata ya Merelani Philemon Oyogo, wameiomba serikali kupitia mamlaka husika kufuatilia mazingira ya kazi wanayopitia wafanyakazi wote katika migodi ya wachimbaji wadogo.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara Francis Masawe amethibitisha kupokea taarifa hizo na kusema tayari wanamshikilia mtu mmoja anayesadikika kuhusika na ukatili huo.
Kwa mujibu wa wenyeji wa eneo hilo wamesema Matukio ya aina hii yamekuwa yakitokea mara kwa mara na kutoa wito kwa serikali na Mamlaka husika kuingilia kati kwa kuchukua hatua stahiki kwa wahusika ili kukomesha vitendo hivyo ambavyo vimeonekana kukithiri katika maeneo haya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu