WANA-POLO waiomba Serikali kuingilia kati vitendo vya unyanyasaji na uzalilishaji dhidi yao.

In Kitaifa
Wakazi wa mji mdogo wa Merelani wameiomba serikali kuingilia kati vitendo vya unyanyasaji na uzalilishaji vinavyoendelea dhidi ya wafanyakazi katika migodi ya wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite maarufu kama WANA-APOLO , baada ya Mfanyakazi kutoka moja ya migodi hiyo kunusurika kufa baada ya kujeruhiwa vibaya kwa kuchomwa moto na mwajiri wake.
Wakazi hao wakiongozwa na Diwani wa kata ya Merelani Philemon Oyogo, wameiomba serikali kupitia mamlaka husika kufuatilia mazingira ya kazi wanayopitia wafanyakazi wote katika migodi ya wachimbaji wadogo.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara Francis Masawe amethibitisha kupokea taarifa hizo na kusema tayari wanamshikilia mtu mmoja anayesadikika kuhusika na ukatili huo.
Kwa mujibu wa wenyeji wa eneo hilo wamesema Matukio ya aina hii yamekuwa yakitokea mara kwa mara na kutoa wito kwa serikali na Mamlaka husika kuingilia kati kwa kuchukua hatua stahiki kwa wahusika ili kukomesha vitendo hivyo ambavyo vimeonekana kukithiri katika maeneo haya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu