WANA-POLO waiomba Serikali kuingilia kati vitendo vya unyanyasaji na uzalilishaji dhidi yao.

In Kitaifa
Wakazi wa mji mdogo wa Merelani wameiomba serikali kuingilia kati vitendo vya unyanyasaji na uzalilishaji vinavyoendelea dhidi ya wafanyakazi katika migodi ya wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite maarufu kama WANA-APOLO , baada ya Mfanyakazi kutoka moja ya migodi hiyo kunusurika kufa baada ya kujeruhiwa vibaya kwa kuchomwa moto na mwajiri wake.
Wakazi hao wakiongozwa na Diwani wa kata ya Merelani Philemon Oyogo, wameiomba serikali kupitia mamlaka husika kufuatilia mazingira ya kazi wanayopitia wafanyakazi wote katika migodi ya wachimbaji wadogo.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara Francis Masawe amethibitisha kupokea taarifa hizo na kusema tayari wanamshikilia mtu mmoja anayesadikika kuhusika na ukatili huo.
Kwa mujibu wa wenyeji wa eneo hilo wamesema Matukio ya aina hii yamekuwa yakitokea mara kwa mara na kutoa wito kwa serikali na Mamlaka husika kuingilia kati kwa kuchukua hatua stahiki kwa wahusika ili kukomesha vitendo hivyo ambavyo vimeonekana kukithiri katika maeneo haya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu