Wanafunzi Elfu Thelathini (30,000) kunufaika na bilioni 427.

In Kitaifa

ZAIDI ya wanafunzi Elfu Thelathini 30,000 wa vyuo vya elimu ya juu nchini kwa mwaka mpya wa masomo 2017/18, watanufaika na Sh bilioni 427 kutoka Bodi Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB), huku wanufaika hao wakiwekwa kwenye mikondo mitatu.

Akizungumza na Vyombo vya habari , Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul –Razaq Badru amesema kwa mwaka huu wanufaika wasiopungua elfu thelathini, watapata mikopo ya elimu kulingana na fani walizochagua kusoma.

Akifafanua idadi na kiwango cha mkopo kitakachotolewa kwa kila mkondo kulingana na fani watakazosoma, ambapo amesema bodi imepanga mikondo mitatu ya mikopo.

Mkondo wa kwanza utawahusu wanafunzi wa fani za afya, sayansi ya elimu na hesabu, ambapo kundi hilo litapata asilimia 40 ya mkopo huo ambao ni sawa na Sh bilioni 170.8.

Badru amesema kundi hilo ndilo litapata mkopo mkubwa kuliko makundi mengine kutokana na fani hizo kuwa adimu na zina mahitaji makubwa ya soko nchini hasa kwa kuwapata wataalamu watakaosaidia taifa kwenye sekta za afya, sayansi na elimu.

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu