Wanafunzi wa shule ya msingi ya Kenyatta Golf Course Academy jijini Nairobi, waliwashangaza wengi baada ya kuyaweka madawati barabarani mapema leo na kusababisha msongamano mkubwa wa magari.

In Kimataifa

Wanafunzi wa shule ya msingi ya Kenyatta Golf Course Academy jijini Nairobi, waliwashangaza wengi baada ya kuyaweka madawati barabarani mapema leo na kusababisha msongamano mkubwa wa magari.

Wanafunzi hao, wakiwa kwenye sare zao rasmi za shule, waliimba na kujipanga kwa sehemu mbalimbali za barabara.

Walimu na wazazi wao nao walijiunga na wanafunzi wakiimba, “tunataka shule yetu, tunahitaji kutumia shule yetu”.

Shule hiyo inadaiwa kubomolewa wikendi kufuatia mzozo wa ardhi iliyotumika kujenga shule hiyo.

Wanafunzi hao wliondoka barabarani baadaye kwa hiari yao wakiwa na matumaini hali hiyo itasuluhishwa.

Zaidi ya shule elfu 24 za umma hazina hatimiliki ya ardhi zinazotumika na shule hizo na hilo limetajwa kutishia elimu ya watoto kwani shule 11,000 zimo hatarini kubomolewa au kunyakuliwa.

Maelfu ya watoto kutoka jamii maskini huenda wakakosa masomo kutokana na hali hiyo.

 

Walimu wa shule hiyo wameeleza wasiwasi wao kwani hatua hiyo imewaathiri kwa kuwaacha bila ajira

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu