Wanafunzi wa shule ya msingi ya Kenyatta Golf Course Academy jijini Nairobi, waliwashangaza wengi baada ya kuyaweka madawati barabarani mapema leo na kusababisha msongamano mkubwa wa magari.

In Kimataifa

Wanafunzi wa shule ya msingi ya Kenyatta Golf Course Academy jijini Nairobi, waliwashangaza wengi baada ya kuyaweka madawati barabarani mapema leo na kusababisha msongamano mkubwa wa magari.

Wanafunzi hao, wakiwa kwenye sare zao rasmi za shule, waliimba na kujipanga kwa sehemu mbalimbali za barabara.

Walimu na wazazi wao nao walijiunga na wanafunzi wakiimba, “tunataka shule yetu, tunahitaji kutumia shule yetu”.

Shule hiyo inadaiwa kubomolewa wikendi kufuatia mzozo wa ardhi iliyotumika kujenga shule hiyo.

Wanafunzi hao wliondoka barabarani baadaye kwa hiari yao wakiwa na matumaini hali hiyo itasuluhishwa.

Zaidi ya shule elfu 24 za umma hazina hatimiliki ya ardhi zinazotumika na shule hizo na hilo limetajwa kutishia elimu ya watoto kwani shule 11,000 zimo hatarini kubomolewa au kunyakuliwa.

Maelfu ya watoto kutoka jamii maskini huenda wakakosa masomo kutokana na hali hiyo.

 

Walimu wa shule hiyo wameeleza wasiwasi wao kwani hatua hiyo imewaathiri kwa kuwaacha bila ajira

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu