Wanafuzi 3 waliokua wakipata matibabu Marekani kurejea Nchini ijumaa.

In Kitaifa

Wanafunzi 3 wa Shule ya Msingi ya Lucky Vincent ya mkoani Arusha waliojeruhiwa katika ajali ya basi Mei 6 mwaka huu, wanatarajia kuwasili nchini Ijumaa kutoka nchini Marekani walikokuwa wakipata matibabu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyoandikwa na Mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu,watoto hao wanatarajiwa kuwasili nchini Ijumaa saa 3 asubuhi, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro KIA.

Wanafunzi hao ni Dorin Mshana, Sadia Awadhi na Wilson Tarimo, ambao walipelekwa nchini humo Mei 14 mwaka huu, kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Mercy Medical iliyoko Sioux City.

Nyalandu ambaye ni mmoja wa waasisi wa Taasisi ya Stem iliyoratibu safari ya majeruhi hao kwenda Marekani, amewaomba watanzania kujitokeza kwa wingi kuwapokea watoto hao ijumaa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu