Wanajeshi 39 wa AU wadaiwa kuuawa na Al-shabaab

In Kimataifa

Kundi la wapiganaji wa Kiislamu wenye itikadi kali la Al Shabaab limedai kwamba limewauwa wanajeshi 39 wa kikosi cha Umoja wa Afrika baada ya kuwavamia katika jimbo la Lower Shabelle ingawa madai hayo hayajathibitishwa.

Wapiganaji hao wa Al Shabaab waliushtukiza msafara wa jeshi la Umoja wa Afrika umbali wa kilomita 150 kusini magharibi kutoka mji mkuu wa Mogadishu.

Kundi hilo la kigaidi linapigana ili kuwaondoa wanajeshi wa kulinda amani wa kikosi cha Umoja wa Afrika.

Vilevile wanataka kuing’oa serikali ya Somalia inayoungwa mkono na nchi za Magharibi.

Umoja wa Afrika una wanajeshi wapatao elfu ishirini wanaopambana na Al Shabaab pamoja na kuiunga mkono serikali ya Somalia.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu