Wananchi wamelalamikia kiwango cha juu cha gharama za viingilio kwenye Maonesho ya 41 ya Bisahara.

In Kitaifa
Wananchi wamelalamikia kiwango cha juu cha gharama za viingilio kwenye Maonesho ya 41 ya Bisahara ya Kimataifa ya Dar es salaam, maarufu kama sabasaba yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Barabara ya Kilwa kwamba ni vikubwa ikilinganishwa na hali ya maisha ya wakati huu.
Wakizungumza na wanahabari wananchi hao wamesema gharama hiyo ya kiingilio cha juu cha shilingi 4000 za kitanzania ni kubwa ikilinganishwa na shilingi 2500 za mwaka jana, hali ambayo imesababisha wengi kutoweza kumudu kutokana na kile walichodai hali ngumu ya maisha iliyopo kwa sasa .
Baada ya Malalamiko hayo wanahabari walilifanikiwa kuzungumza na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusinao wa Umma kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara TANTRADE ambao ndio waandaji wa Maonesho hayo.
Hata hivyo Kwa mujibu wa Tantrade, hakutakuwa na mabadiliko ya gharama kwa siku tano za nyongeza za maonesho hayo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu