Wanaotaka kuendeleza Mapigano Sudan sasa waone aibu-Mamabolo

In Kimataifa

Kwa kuwa hali ya amani na usalama nchini Sudan imeanza kubadilika na kuwa nzuri, sasa ni wakati muafaka kwa pande zote kinzani kutumia fursa hiyo na kumaliza kabisa mzozo ulioanza nchini humo mwaka 2003.

 

Mkuu wa ujumbe wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika, huko Darfur, UNAMID Jeremiah Mamabolo amesema hayo akizungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa akisema kuwa fursa ya sasa ni ya kipekee na haijawahi kutokea.

 

Amesema sitisho la mapigano linazingatiwa na wale wanaotaka kupigana wanapaswa kuona aibu kwa kuwa mazingira muafaka ya kumaliza mzozo huo ni pamoja na …

 

“Kuondolewa kwa vikwazo kulikofanywa na Marekani, na maazimio chanya kutoka mkutano wa viongozi wa Muungano wa Afrika kuhusu Sudan na ukanda mzima ambapo watu wanawatakia mema wasudan. Hivyo basi wao wenyewe wanatakiwa kutambua hilo na kumaliza machungu haya ambayo yamewafika wananchi kutokana na vita hivi.”

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu