Wanawake nchini Iran wazuiwa kuhudhuria mechi kati ya Iran na Syria.

In Kimataifa, Michezo

 

Wanawake nchini Iran walizuiwa kuingia uwanja wa taifa wa nchi hiyo, ambapo timu yao ya taifa ilikuwa ikicheza mechi ya kufuzu kombe la dunian dhidi ya Syria, licha ya kuwa na tiketi.

Wanawake hao walikusanyika nje ya uwanja wa Azadi mjini Tehran, kulalamika wakati waliamrishwa kuondoka huku wanawake raia Syria wakiruhusiwa kuingia uwanjani bila tatizo lolote baada ya kuonyesha paspoti zao.

Emeelezwa kuwa wanawake wamepigwa marufuku nchini humo kuhudhuria mechi za kandanda ya wanaume.

Wanawake kadha walikuwa wamenunua tiketi kwa njia ya mtandao, wiki moja mapema kabla ya mechi.

Lakini shiriko la kandanda nchini Iran lilisema kuwa tiketi hizo ziliuzwa kimakosa, na kuahidi kuwarejeshea pesa wanawake ambao walikuwa tayari wamezinunua.

Wale waliokuwa na tiketi hata hivyo waliamua kuelekea uwanjani jana Jumanne wakitaka kujaribu ikiwa wangeruhusiwa kuingia, hata hivyo hawakuruhusiwa.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu