Wanawake nchini Iran wazuiwa kuhudhuria mechi kati ya Iran na Syria.

In Kimataifa, Michezo

 

Wanawake nchini Iran walizuiwa kuingia uwanja wa taifa wa nchi hiyo, ambapo timu yao ya taifa ilikuwa ikicheza mechi ya kufuzu kombe la dunian dhidi ya Syria, licha ya kuwa na tiketi.

Wanawake hao walikusanyika nje ya uwanja wa Azadi mjini Tehran, kulalamika wakati waliamrishwa kuondoka huku wanawake raia Syria wakiruhusiwa kuingia uwanjani bila tatizo lolote baada ya kuonyesha paspoti zao.

Emeelezwa kuwa wanawake wamepigwa marufuku nchini humo kuhudhuria mechi za kandanda ya wanaume.

Wanawake kadha walikuwa wamenunua tiketi kwa njia ya mtandao, wiki moja mapema kabla ya mechi.

Lakini shiriko la kandanda nchini Iran lilisema kuwa tiketi hizo ziliuzwa kimakosa, na kuahidi kuwarejeshea pesa wanawake ambao walikuwa tayari wamezinunua.

Wale waliokuwa na tiketi hata hivyo waliamua kuelekea uwanjani jana Jumanne wakitaka kujaribu ikiwa wangeruhusiwa kuingia, hata hivyo hawakuruhusiwa.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu