Baadhi ya vijana wa kike na wa kiume jijini Arusha wamejitoa kwenye makundi ya mtaani na kufanya kazi ya kuosha magari maarufu kama car wash ili waweze kujikwamua kimaisha
Walizungumza na vyombo vya habari wakati walipotembelewa kwenye kituo cha uptown carwash vijana hao wamesema kuwa kumekuwepo na changamoto kubwa ya kupata ajira na hii inatokana na vijana wengi kuchagua kazi na kuwa wavivu wa kufanya kazi
Kwa upande wake mwanadada Neema Lyimo ambae ni mtoto wa kike ambae ameamua kujitoa na kufanya kazi hiyo ambayo imekuwa ikiachiwa watoto wa kike amesema kuwa ameweza kujikwamua kimaosha kwa kufanya mambo mengi ya maendeleo kama kulipa kodi ya nyumba na matumizi mengine madogo madogo
Nae Mkurugenzi wa UPTOWN CARWASH Joachim Mushi amesema kuwa lengo la kufungua hiyo ni ili kuweza kuwapa vijana ajira na aweze kuifikia jamii kwa urahisi kwa kuwa huduma hiyo ni muhimu na inaweza kuleta manufaa makubwa kwa vijanaInsert mkurugenzi.
Amesema licha ya kufungua fursa hiyo lakini bado kuna changamoto wanazokabiliana nazo zikiwemo ushindani wa biashara hiyo kwa kuwa sehemu za kuoshea magari jijini Arusha zimekuwa ni nyingi na hivyo wateja kukosa kushindwa kujua ni sehemu gani ina ubora
Hata hivyo amewataka vijana wa kike kutochagua kazi na badala yake wajitume ikiwa ni pamoja na kufanya biashara mbalimbali za ujasiriamali ili waweze kujenga maisha yaliyo bora kwa sasa na badae