Washukiwa 25 wanaodaiwa kupanga njama za mapinduzi wakamatwa Ujerumani

In Kimataifa

Maelfu ya polisi leo wamefanya msururu wa misako kote Ujerumani wa washukiwa wa siasa kali za mrengo wa kulia wanaodaiwa kupanga njama ya kuipindua serikali kwa kutumia silaha. Waendesha mashitaka wa serikali wamesema karibu maafisa 3,000 walifanya misako hiyo ya kile kinachofahamika kama vuguvugu la Reich Citizens.

Baadhi ya wanachama wa kundi hilo wanapinga katiba ya Ujerumani iliyoandikwa baada ya vita na wametoa mwito wa kuangushwa kwa serikali. Waendesha mashitaka wanasema raia 22 wa Ujerumani wamekamatwa kwa kushukiwa kuwa waanachama wa kundi la kigaidi. Watu wengine watatu, akiwemo raia wa Urusi, wanatuhumiwa kuliunga mkono kundi hilo.

Jarida la kila wiki la Der Spiegel limeripoti kuwa maeneo yaliyofanyiwa msako yanajumuisha kambi ya kitengo maalum cha vikosi vya Ujerumani KSK katika mji wa kusini magharibi wa Calw. KSK katika siku za nyuma ilituhumiwa kwa madai kuwa baadhi ya wanajeshi wake wanajihusisha na siasa kali za mrengo wa kulia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu