Wastani wa wanafunzi saba hupewa ujauzito kila mwezi katika wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro

Wastani wa wanafunzi saba hupewa ujauzito kila mwezi katika wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro kwa kipindi cha miezi sita iliyopita, jambo ambalo linatishia mustakabali wa elimu ya mtoto wa kike wilayani humo.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Mkuu wa wilaya hiyo, Agnes Hokororo hadi kufikia Juni mwaka huu jumla ya wanafunzi 42 wa shule za msingi na sekondari wamekatisha masomo baada ya kupata ujauzito.

Takwimu hizo zimetajwa ni kwa kipindi hadi kufikia shule hizo zinafungwa mwezi mmoja uliopita ambapo mipango imewekwa kufanyiwa tena kwa vipimo kwa wanafunzi wote wa kike mara baada ya kufunguliwa kwa shule za msingi na sekondari Julai 3 mwaka huu.

Amesema pamoja na mimba za utotoni lakini pia katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Julai mwaka huu kumeripotiwa matukio 25 ya ubakaji na nane ya ulawiti, jambo ambalo linaashiria wananchi kukiuka utii wa sheria

 

 

 

 

 

Exit mobile version