Watoto 27 wauawa kwenye shambulio la Idlib-UNICEF

In Kimataifa

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Alhamisi limethibitisha kwamba watoto 27 wamepoteza maisha kwenye shambulio la Idlib Syria Jumanne. Watu wengine 546 miongoni mwao watoto wengi wamejeruhiwa na idadi ya waliokufa inatarajiwa kuongezeka.

Mauji ya watoto Syria hayawezi kuendelea kuruhusiwa amesema mkurugenzi wa kikanda wa Syria Geert Cappelaere, akizitaka pande zote kwenye mzozo na walio na ushawishi katika vita hivyo kukomesha mara moja jinamizi hilo.

UNICEF na washirika wengine wanaendelea kusaidia waathirika wa shambulio hilo kwa kuwezesha kliniki tatu na hospitali nne ambazo zinatoa huduma ya kwanza, pia wanasaidia magari 9 ya kubeba wagonjwa ili kuwasafirisha hadi hospitali za jirani.

UNICEF pia inapeleka msaada muhimu wa vifaa vya afya na kushirikiana na wahudumu wa afya kuelimisha kuhusu huduma za afya za kukabiliana na mashambulizi ya kemikali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu