Watu 1,000 waandamana mjini Moscow

In Kimataifa
Kiasi ya watu 1,000 wameandamana hapo jana mjini Moscow kupinga hatua ya serikali kudhibiti matumizi ya mtandao wa Intaneti.
Urusi katika miaka ya hivi karibuni imekua ikichukua hatua za kudhibiti matumizi ya Intaneti pamoja na kuwafungulia mashitaka watu kadhaa kwa makosa yanayohusiana na matumizi ya mitandao ya kijamii.
Waandamanji walisikika wakipaza sauti kupinga hatua hiyo na polisi nchini humo wanasema kiasi ya watu 800 walishiriki maandamano hayo yaliyoandaliwa na chama cha upinzani kilichokuwa kikiongozwa na Waziri Mkuu wazamani Mikhail Kasyanov.
Mwandishi wa habari wa shirika la habari la AFP amekadiria watu waliojitokeza kwenye maandamano hayo kuwa kati ya 1,000 na 1,500.
Tangu Januari mosi makampuni ya intaneti nchini humo yametakiwa kutunza ujumbe wa mawasiliano binafsi kwa ajili ya kuwasilisha katika vyombo vya serikali pindi utakapohitajika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu