Watu 1,000 waandamana mjini Moscow

In Kimataifa
Kiasi ya watu 1,000 wameandamana hapo jana mjini Moscow kupinga hatua ya serikali kudhibiti matumizi ya mtandao wa Intaneti.
Urusi katika miaka ya hivi karibuni imekua ikichukua hatua za kudhibiti matumizi ya Intaneti pamoja na kuwafungulia mashitaka watu kadhaa kwa makosa yanayohusiana na matumizi ya mitandao ya kijamii.
Waandamanji walisikika wakipaza sauti kupinga hatua hiyo na polisi nchini humo wanasema kiasi ya watu 800 walishiriki maandamano hayo yaliyoandaliwa na chama cha upinzani kilichokuwa kikiongozwa na Waziri Mkuu wazamani Mikhail Kasyanov.
Mwandishi wa habari wa shirika la habari la AFP amekadiria watu waliojitokeza kwenye maandamano hayo kuwa kati ya 1,000 na 1,500.
Tangu Januari mosi makampuni ya intaneti nchini humo yametakiwa kutunza ujumbe wa mawasiliano binafsi kwa ajili ya kuwasilisha katika vyombo vya serikali pindi utakapohitajika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu