Watu 20 wamekamatwa na magunia ya Bangi.

In Kitaifa

WATU 20 wamekamatwa kwa kukutwa na shehena ya bangi gunia 168 katika kitongoji cha Engendeko, Kijiji cha Losinoni wilayani Arumeru mkoani Arusha.

Akithibitisha kukamatwa kwa shehena hiyo ya bangi Kamishna wa Intelijensia wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Fredrick Kibute amesema ofisi yake ilishirikiana na askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kutoka Oljoro ili kufanikisha kazi hiyo.

Aisha amesema kuwa walipata taarifa kutoka kwa raia wema na wiki iliyopita tukatuma kikosi maalumu, kwa ajili ya uchunguzi na baada ya kupata taarifa za uwepo wa bangi hiyo na kupanga  safu ya kikosi kazi kwa ajili ya kuja Arusha kukamata bangi hiyo ambayo awali wananchi hao waligomea uongozi wa wilaya baada ya kutakiwa kukisalimisha.

Kamishina Kibute ametumia fursa hiyo kuwaonya wananchi wa Wilaya ya Arumeru kuacha mara moja tabia hiyo ya kulima bangi, na kuwataka wasome alama za nyakati badala ya kufanya kilimo hicho kwa mazoea.

Serikali ya Wilaya ya Arumeru tangu Agosti mwaka jana ilianza kupambana na kudhibiti kilimo cha bangi katika kata 14 na vijiji 22, ambavyo vilikuwa vinategemea kilimo cha bangi kama kitega uchumi cha kujipatia kipato.

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu