Watu 3,383 wameuawa huko kasai, kanisa katoliki wamebaini.

In Kimataifa
Kanisa Katoliki nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo linasema watu 3,383 wameuawa katika jimbo la Kasai katika jimbo la Kasai tangu mwezi Oktoba mwaka uliopita.
Shirika la Habari la Uingereza la Reuters, limeripoti kuwa takwimu hizo zimepatikana baada ya utafiti wa Kanisa hilo.
Ripoti hii inakuja baada ya Umoja wa Mataifa nao kusema kuwa watu waliopoteza maisha katika kipindi hicho ni zaidi ya 400 baada ya makaburi 20 ya halaiki kugundulika katika jimbo hilo.
Utafiti wa Kanisa Katoliki pia umebaini kuwa vijiji 10 vimeteketezwa moto katika jimbo hilo.
Waasi wa Kamwina Nsapu wamekuwa wakikabiliana na wanajeshi wa serikali katika jimbo hilo.
Maelfu ya watu katika jimbo hilo wameyakimbia makwao huku wengine wakikimbilia nchi jirani ya Angola.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu