Watu 3,383 wameuawa huko kasai, kanisa katoliki wamebaini.

In Kimataifa
Kanisa Katoliki nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo linasema watu 3,383 wameuawa katika jimbo la Kasai katika jimbo la Kasai tangu mwezi Oktoba mwaka uliopita.
Shirika la Habari la Uingereza la Reuters, limeripoti kuwa takwimu hizo zimepatikana baada ya utafiti wa Kanisa hilo.
Ripoti hii inakuja baada ya Umoja wa Mataifa nao kusema kuwa watu waliopoteza maisha katika kipindi hicho ni zaidi ya 400 baada ya makaburi 20 ya halaiki kugundulika katika jimbo hilo.
Utafiti wa Kanisa Katoliki pia umebaini kuwa vijiji 10 vimeteketezwa moto katika jimbo hilo.
Waasi wa Kamwina Nsapu wamekuwa wakikabiliana na wanajeshi wa serikali katika jimbo hilo.
Maelfu ya watu katika jimbo hilo wameyakimbia makwao huku wengine wakikimbilia nchi jirani ya Angola.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu