Takribani watu 29 wameuawa katika siku tatu za ghasia kati ya makundi yanayomiliki silaha katika eneo lenye utovu wa usalama mashariki mwa DRC,maafisa wamethibitisha.
Makundi mawili yanayomiliki silaha yanapambana kudhibiti kijiji cha Bweru katika jimbo la Kivu ya kaskazini,ambalo limekuwa likishuhudia umwagaji damu unaotakana na mapigano ya kikabila.
Kwa mujibu wa kiongozi wa eneo hilo Dieudonne Tshishiku,tangu siku ya jumatano makundi ya wapiganaji wa Mai mai Nyatura yamekabiliana kudhibiti kijiji na kusababisha vifo vya watu 29.
Kiongozi huyo amesema ghasia hizo bado zinaendelea katika kijiji cha Bweru na maeneo ya jirani na kulitaka jeshi la Congo kuingilia kati kukomesha vurugu na kuwarejesha raia waliokimbia makazi yao.
Afisa mmoja wa shirika lisilo la kiserikali amesema pasipo kutaja jina lake kuwa miongoni mwa watu 29 waliouawa ni wapiganaji 11 na kuongeza kuwa raia pia ni miongoni mwa waliouawa
