Watu Takribani 29 wauawa Mashariki mwa DRC.

In Kimataifa

Takribani watu 29 wameuawa katika siku tatu za ghasia kati ya makundi yanayomiliki silaha katika eneo lenye utovu wa usalama mashariki mwa DRC,maafisa wamethibitisha.

Makundi mawili yanayomiliki silaha yanapambana kudhibiti kijiji cha Bweru katika jimbo la Kivu ya kaskazini,ambalo limekuwa likishuhudia umwagaji damu unaotakana na mapigano ya kikabila.

Kwa mujibu wa kiongozi wa eneo hilo Dieudonne Tshishiku,tangu siku ya jumatano makundi ya wapiganaji wa Mai mai Nyatura yamekabiliana kudhibiti kijiji na kusababisha vifo vya watu 29.

Kiongozi huyo amesema ghasia hizo bado zinaendelea katika kijiji cha Bweru na maeneo ya jirani na kulitaka jeshi la Congo kuingilia kati kukomesha vurugu na kuwarejesha raia waliokimbia makazi yao.

Afisa mmoja wa shirika lisilo la kiserikali amesema pasipo kutaja jina lake kuwa miongoni mwa watu 29 waliouawa ni wapiganaji 11 na kuongeza kuwa raia pia ni miongoni mwa waliouawa

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu