Watu wa 3 wamefariki dunia jana na wengine 3 kujeruhiwa baada ya gari aina ya Mitsubish Fuso tipa lenye namba za usajli T 892 BRH walilokuwa wakisafinalo waki tokea kijiji ncha kisomachi kuelekea uchira likiwalimebeba mawe kuacha njia na kugonga nyumba kisha kupinduka katika kijiji cha uchira wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro.
Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wamesema gari hilo lilikuwa kwenye mwendo kasi ,kwenye barabara itokayo shule ya sekondari uchira majira ya saa tisa ala siri, kisha likavuka barabara kuu itokakayo Moshi kueleke Dar es salaam nakug onga nyumba ya Samwel Koka na kujeruhi watoto 2 ndani ya nuymba hiyo.
Nae mwanamazingira wa shule ya sekondari chira Hajii Msofe amesemaa awali lori hilo lilikuwa likipakiw a mawe kwenye shamba la shule hilobila idhini ya shule na kwamba alitoa taarifa kwa mwalimu mkuu, nakujaribu fuatilia ,walikutana na gari hilo na dereva alikataa kusimama na kuwapita kwa kasi.
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Koka Moita amesema ajali imetokana na mwendo kasi, auliyosababisha dereva alishin dwa kumudu gari hilo ambalo lilikuwa limebeba mawe kisha kugonga nyumba na kupinduka, na kusababisha vifo cha watu watatu na majeruhi watatu.
Kamanda Moita amewataja waliyofariki ni kuwa ni dereva wagari hilo Francis Ngowi na ambria Andason John pamoja na abiria mmoja ambaye bado jina leke halij afahamika pia kulikuwepo na majeruhi watatu Danieli august ambaye ni abiria,Jacklin Eliam na Irine Samwel ambao ni watoto wa mwenye nyumba.
Kwamujibu wa taarifa za kamanda Moita miili ya marehemu imehifadhiwa katika hosptali ya rufaa yakcmc na majeruhi pia wanaendele kupatiwa matib abu katika hosptali hiyo.
