Watu wanne wauawa kwenye ghasia mjini Nairobi, Kenya.

In Kimataifa

Takriban watu wanne wamethibitishwa kuuawa wakati wa mashambulizi kwenye mtaa wa Mathare mjini Nairobi nchini Kenya.

Wakaazi wa mtaa huo wa mabanda wanadai kuwa makundi yaliyokuwa yamejihami kwa panga na silaha zingine yalivamia mtaa huo na kuwaua watu hao ambapo pia waliharibu mali.

Polisi wanasema kuwa wanachunguza kisa hicho na nia yake.

Wakaazi wanasema waliamka kwa mshangao asubuhi walipopata miili ya watu wanne iliyokuwa na majeraha.

Kuuliwa kwa watu hao kumesababisha ghasia kusambaa hadi mitaa iliyo karibu huku polisi wakikabiliana na wale waliokuwa wakilalamikia mauaji hayo.

Kamanda wa polisi mjini Nairobi Japheth Koome alithibitisha mauaji hayo na kusema kuwa uchunguzi unafanywa, lakini akatupilia mbali madai kuwa yamesababishwa na ghasia za kikabila kufuatia hali ya kisiasa iliyopo sasa.

Mauaji hayo yanatokea siku moja baada ya watu wengine watano kuuwa wakati wa shughuli ya kumkaribisha kinara wa upinzani ambaye amekuwa ziarani Ulaya na Marekani.

Polisi wanasema kuwa wale waliouawa walikuwa ni wezi waliopigwa na watu waliokuwa na hasira.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu