Watu wanne wauawa kwenye ghasia mjini Nairobi, Kenya.

In Kimataifa

Takriban watu wanne wamethibitishwa kuuawa wakati wa mashambulizi kwenye mtaa wa Mathare mjini Nairobi nchini Kenya.

Wakaazi wa mtaa huo wa mabanda wanadai kuwa makundi yaliyokuwa yamejihami kwa panga na silaha zingine yalivamia mtaa huo na kuwaua watu hao ambapo pia waliharibu mali.

Polisi wanasema kuwa wanachunguza kisa hicho na nia yake.

Wakaazi wanasema waliamka kwa mshangao asubuhi walipopata miili ya watu wanne iliyokuwa na majeraha.

Kuuliwa kwa watu hao kumesababisha ghasia kusambaa hadi mitaa iliyo karibu huku polisi wakikabiliana na wale waliokuwa wakilalamikia mauaji hayo.

Kamanda wa polisi mjini Nairobi Japheth Koome alithibitisha mauaji hayo na kusema kuwa uchunguzi unafanywa, lakini akatupilia mbali madai kuwa yamesababishwa na ghasia za kikabila kufuatia hali ya kisiasa iliyopo sasa.

Mauaji hayo yanatokea siku moja baada ya watu wengine watano kuuwa wakati wa shughuli ya kumkaribisha kinara wa upinzani ambaye amekuwa ziarani Ulaya na Marekani.

Polisi wanasema kuwa wale waliouawa walikuwa ni wezi waliopigwa na watu waliokuwa na hasira.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu