Watu wasiopungua 12 wameuawa jana katika shambulio la kujitoa muhanga na risasi dhidi ya mgahawa maarufu katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.

In Kimataifa

Watu wasiopungua 12 wameuawa jana katika shambulio la kujitoa muhanga na risasi dhidi ya mgahawa maarufu katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.

Afisa wa polisi Ali Hassan amesema mripuaji wa kujitoa muhanga alijiripua kwenye gari katika lango la mgahawa wa Bosh Treats, ambao pia unahudumu kama hoteli, na kuuwa walinzi na raia.

Mripuko huo pia ulishambulia kwa sehemu mgahawa wa jirani.

Maafisa usalama wanaamini washambuliaji wenye silaha pia walijigawa katika makundi mawili, na kuvamia migahawa yote, na kuchukuwa watu mateka katika jengo la pili. Kundi la Al-Shabaab limedai kuhusika na shambulizi hilo kupitia kituo chake cha redio cha Andalus.

Watu kadhaa waliokolewa katika mgahawa wa kwanza, kwa mujibu wa afisa usalama wa Somalia Mohammed Hassan.

Miongoni mwao walikuwemo wageni kutoka Kenya na Somalia waliokuwa wanafanyakazi katika mgahawa huo.

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu