Watu wasiopungua 12 wameuawa jana katika shambulio la kujitoa muhanga na risasi dhidi ya mgahawa maarufu katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.

In Kimataifa

Watu wasiopungua 12 wameuawa jana katika shambulio la kujitoa muhanga na risasi dhidi ya mgahawa maarufu katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.

Afisa wa polisi Ali Hassan amesema mripuaji wa kujitoa muhanga alijiripua kwenye gari katika lango la mgahawa wa Bosh Treats, ambao pia unahudumu kama hoteli, na kuuwa walinzi na raia.

Mripuko huo pia ulishambulia kwa sehemu mgahawa wa jirani.

Maafisa usalama wanaamini washambuliaji wenye silaha pia walijigawa katika makundi mawili, na kuvamia migahawa yote, na kuchukuwa watu mateka katika jengo la pili. Kundi la Al-Shabaab limedai kuhusika na shambulizi hilo kupitia kituo chake cha redio cha Andalus.

Watu kadhaa waliokolewa katika mgahawa wa kwanza, kwa mujibu wa afisa usalama wa Somalia Mohammed Hassan.

Miongoni mwao walikuwemo wageni kutoka Kenya na Somalia waliokuwa wanafanyakazi katika mgahawa huo.

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu