Watu wasubiri hatua za jeshi Zimbabwe.

In Kimataifa

Watu nchini Zimbabwe wanasubiri kuona hatua ambazo jeshi litachukua baada ya kutwaa madaraka ya nchi hiyo.

Rais Robert Mugabe yuko katika kizuizi cha nyumbani mjini Harare lakini ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa mke wake Grace ambaye alikuwa anataka kumrithi akimekimbia kwenda Namibia

Hatua za kijeshi zilifuatia kufutwa kwa Makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa ambayr ni hasimu mkubwa wa Bi Grace Mugabe.

Mahala alipo Mnangagwa pia hapajulikani.

Lakini mzozo kuhusu ni nani anaweza kumrithi Mugabe kati ya Bi Grace Mugabe na Bwa Mnangagwa umekigawanya chama cha Zanu-PF miezi ya hivi karibuni.

Nchi za Jumuia ya maendeo ya kusini mwa Afrika (SADC) zinatarajiwa kufanya mkutano wa dharura nchini Botswana leo Alhamisi.

Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe Tendai Biti, aliiambia BBC kuwa anataka kuona serikali ya mpito madarakani.

Siku ya Jumatano wanajeshi wakiwa na magari ya jeshi walilizinga bunge na majengo mengine makuu ya serikali.

Saa kadha baadaye walichukua udhibiti wa makao ya kituo cha habari cha serikali ZBC na kutangaza kuwa walikuwa wanawalenga waalifu wanamzunguka Rais Mugabe.

Hata hivyo meja Jenerali Sibusiso Moyo alikana kuwa hakkukuwa na mapinduzi wa kijeshi.

Alisema kuwa Mugabe na familia yake walikuwa salama.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu