Watu wawili wameuwawa na wengine wanne wamejeruhiwa vibaya huko Venezuela.

In Kimataifa
Watu wawili wameuwawa na wengine wanne wamejeruhiwa vibaya hapo jana katika ghasia za nchini Venezuela wakati upinzani wa kisiasa ulipoitisha kura ya maoni isiyo rasmi ya kupinga mipango ya Rais Nikolas Maduro ya kuiandika tena katiba ya nchi.
Kulingana na msemaji mkuu wa upinzani, watu wenye silaha waliokuwa wamepanda pikipiki walikishambulia kituo cha kupigia kura katika mji wa Catia, kaskazini magharibi mwa mji mkuu wa Caracas.
Taifa hilo lenye utajiri wa mafuta linakabiliwa na mgogoro mbaya wa kiuchumi kuwahi kutokea, huku kukiwa na uhaba wa mahitaji kadhaa ya msingi pamoja na mfumko wa bei wa hali ya juu.
Zaidi ya watu 90 wameuwawa katika maandamano ya kila siku ya kuipinga serikali iliyopo madarakani yaliyoanza tokea mwezi Aprili mwaka huu.
Maduro ambaye amekataa kuachia madaraka, pia ameitisha kura ya maoni baadaye mwezi huu ya kuteua kamati maalumu itakayoandika upya katiba ya taifa hilo la Amerika Kusini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu