Watu wenye silaha wameshambulia ofisi ya mkuu wa mashtaka na kituo cha polisi kwenye mji mkuu wa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo Kinshasa na kusababisha wafungwa kadha kutoroka

In Kimataifa
Watu wenye silaha wameshambulia ofisi ya mkuu wa mashtaka na kituo cha polisi kwenye mji mkuu wa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo Kinshasa na kusababisha wafungwa kadha kutoroka
Afisa mmoja wa polisi ameripotiwa kuuawa na wengine wanne kujeruhiwa katika tukio hilo huku kukiwa na ripoti tofauti kuhusu ni wafungwa wangapi walifanikiwa kutoroka.
Hakimu katika wilaya Matete mashariki mwa mji mkuu Kinshasa ameiambia AFP kuwa watu wenye silaha wasiojulikana walishambulia ofisi ya mahakama siku ya Ijumaa usiku, kuchoma magari kadhaa yaliyokuwa yameegesha katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa Redio inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa, Radio Okapi, wafungwa 17 walitoroka, wengi kutoka katika kituo cha polisi.
Aidha Mtandao mmoja wa habari nchini DRC Politico, unasema kuwa washambuliajia walikuwa ni wanachama wa Bunda dia Kongo kundi la kidini lenye mtazamo wa siasa.
Serikali inalishutumu kundi hilo kufuatia shambulizi lililotokea katika gereza kuu la Kinshasa mwezi uliopita ambapo mamia ya wafungwa walitoroka.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu