Watu zaidi 50 wauawa kwa shambulio la Boko Haram.

In Kimataifa

Idadi ya vifo inayotokana na shambulio la kundi la Boko Haram dhidi ya timu ya utafutaji wa mafuta kaskazini mashariki mwa Nigeria mapema wiki hii imeongezeka hadi kufika watu zaidi ya 50.

Likinukuu vyazo vya kijeshi, kitabibu na makundi ya kutoa misaada ya kiutu, shirika la habari la Kifaransa la AFP limesema idadi ya vifo ni kubwa kuliko ile iliyotolewa na maafisa wa serikali, na kwamba maiti bado zinaendele kuwasili katika kitio cha afya.

Shambulio hilo la Jumatano iliyopita lililenga timu ya Shirika la Petroli la Kitaifa la Nigeria na wanajiolojia waliokuwa katika eneo la Ziwa Chad. Hapo jana, jeshi la Nijeria limesema kwamba watu watano kutoka katika kundi hilo wameuwawa, pamoja na wanajeshi kadhaa.

Eneo la kaskazini mashariki mwa Nigeria kwa miaka minane sasa limekuwa likishambuliwa na uasi wa kundi la misiamamo mikali ya kidini la Boko Haram,ambalo limesababisha vifo vya watu 20,000 na wengine milioni 2.7 kuyahama makaazi yao.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu