Watu zaidi 50 wauawa kwa shambulio la Boko Haram.

In Kimataifa

Idadi ya vifo inayotokana na shambulio la kundi la Boko Haram dhidi ya timu ya utafutaji wa mafuta kaskazini mashariki mwa Nigeria mapema wiki hii imeongezeka hadi kufika watu zaidi ya 50.

Likinukuu vyazo vya kijeshi, kitabibu na makundi ya kutoa misaada ya kiutu, shirika la habari la Kifaransa la AFP limesema idadi ya vifo ni kubwa kuliko ile iliyotolewa na maafisa wa serikali, na kwamba maiti bado zinaendele kuwasili katika kitio cha afya.

Shambulio hilo la Jumatano iliyopita lililenga timu ya Shirika la Petroli la Kitaifa la Nigeria na wanajiolojia waliokuwa katika eneo la Ziwa Chad. Hapo jana, jeshi la Nijeria limesema kwamba watu watano kutoka katika kundi hilo wameuwawa, pamoja na wanajeshi kadhaa.

Eneo la kaskazini mashariki mwa Nigeria kwa miaka minane sasa limekuwa likishambuliwa na uasi wa kundi la misiamamo mikali ya kidini la Boko Haram,ambalo limesababisha vifo vya watu 20,000 na wengine milioni 2.7 kuyahama makaazi yao.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu