watumishi 134 wa Hospitali ya Muhimbili wabainika kuwa na vyeti vya kugushi.

In Kitaifa

Watumishi 134 wa hospitali ya taifa Muhimbili wamebainika kuwa na vyeti vya kughushi ,vya ngazi ya elimu ya sekondari hapa nchini.

Taarifa kutoka kwenye uongozi wa hospitali hiyo imesema , hospitali iliendesha zoezi la uhakiki wa vyeti vya elimu vya sekondari kwa watumishi wake, kwa kushirikiana na baraza la mitihani la Tanzania (NECTA) ,baada ya Agizo la serikali kutaka uhakiki ufanyike kwa watumishi wa Umma.

Idara iliyoathirika zaidi ni idara ya uuguzi ambapo watumishi wake takriban 70 ,wamekutwa na vyeti vya kughushi.

Baadhi ya idara nyingine zilizoguswa kwenye zoezi hilo ni Idara ya tiba watumishi 20, tiba shirikishi watumishi 14, upasuaji watumishi wanne, Idara ya Tehama watumishi 11, rasilimali, ufundi, fedha na mipango.

Kutokana na dosari hizo, uongozi huo umesema watumishi waliobainika wamekosa sifa za kuendelea kuwa watumishi wa umma, hivyo wametakiwa kujiondoa wenyewe kazini kabla ya tarehe 15 mwezi Mei mwaka 2017 ,ili kuepuka kuchukuliwa hatua za kisheria.

Uongozi wa Muhimbili umetoa orodha ya watumishi walioghushi vyeti na kuwataka wakuu wa Idara mbalimbali, kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanaohusika hawaendelei kutoa huduma hospitalini hapo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu