Watumishi 9,932 waliotajwa kuhusika na kughushi vyeti waonywa wanaokusudiwa kukata rufaa ikibainika wameendelea kuidanganya serikali watapata adhabu kubwa zaidi.

In Kitaifa

SERIKALI imewaonya watumishi wa umma waliotajwa kuhusika na kughushi vyeti wapatao 9,932 kwamba wasifanye mzaha na suala hilo na kwamba wanaokusudia kukata rufaa, ikibainika wameendelea kuidanganya serikali, watapata adhabu kubwa zaidi.

Aidha, imebainika kwamba wapo watu wanaopata mamilioni kwa kuwahadaa, walioingia kwenye orodha ya watumishi wenye vyeti feki kwa kutoa kati ya Sh milioni moja hadi Sh milioni nne, ili kuondolewa katika orodha hiyo.

Kwa nyakati tofauti  mjini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Laurean Ndumbaro, wametoa kauli za kuonya kuhusu watumishi hao wenye vyeti feki kuwa wasifanye mzaha na suala hilo.

Akijibu mwongozo bungeni jana, Kairuki amesema wote wenye malalamiko halali, waandike barua kwa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) kupitia kwa waajiri wao kulalamika.

Amesema wanaolalamika kuwa wameonewa huku wanajua kwa uhakika kwamba walighushi vyeti vyao, ikibainika wameendelea kuidanganya serikali watapata adhabu kubwa.

Kairuki amesema taarifa ya uhakiki ilivyotoka Aprili 28, mwaka huu wapo ambao wamekubali na kuachia ofisi kabla ya Mei 15, mwaka huu ambayo ni siku ya mwisho na wengine wanapinga kwamba hawana vyeti feki.

Mapema bungeni, Mbunge wa Viti Maalumu, Conchesta Rwamlaza (CCM) aliomba mwongozo akisema baadhi ya watu wamelazwa hospitalini kutokana na kutajwa kwenye orodha ya watu wenye vyeti feki.

Dk Ndumbaro amesema vyeti hivyo wanaangalia index namba na gamba la vyeti vyenyewe, nakala hizo za vyeti vilivyoskaniwa au nakala laini, zinaweza kutumwa kwa njia ya barua pepe ya Necta na wizara kabla ya Mei 15, mwaka huu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu