Waziri Lukuvi amjibu Sumaye.

In Kitaifa

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe William Lukuvi, amesema mtu yoyote asiyelipa kodi ya ardhi na kuendeleza ardhi hiyo, ni sababu tosha ya kunyang’anywa.

Waziri Lukuvi amebainisha hayo ikiwa imepita siku moja toka aliyekuwa Waziri Mkuu awamu ya tatu Mh Fredrick Sumaye, kudai chanzo cha kupokonywa shamba lake ni siasa tu za yeye kuhama chama cha CCM.

 

Kuhusu mashamba na viwanja kuchukuliwa Waziri Lukuvi amesema kuwa, kila mtu atambue iwe ni kiwanja au shamba kama unatabia ya kutolipa kodi ya ardhi, ni sababu tosha kunyang’anywa shamba lako au ardhi unayomiliki.

 

Waziri Lukuvi amesema imejitokeza kwa watu wachache kuchukua ardhi kubwa kwa miaka mingi kuliko hata uwiano wa uendelezaji wa ardhi hiyo.

 

Kwa upande mwingine Waziri Lukuvi amesema kuwa, serikali imekuwa na huruma kwa miaka mingi kwa wananchi wake, lakini serikali ya uongozi huu wamekubaliana kila mtu afuate sheria anazo paswa kuzifuata.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu