Waziri Mkuu awataka wakuu wa Wilaya kuwachukulia hatua za kisheria watendaji wanaoshindwa kuzingatia sheria za utumishi.

In Kitaifa

     WAZIRI Mkuu wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania KASSIMU MAJALIWA amewataka wakuu wa Wilaya Nchini ,kuwachukulia hatua za kisheria watendaji wote ambao wanashindwa kuzingatia sheria za utumishi, kwa kuvujisha taarifa mbalimbali za Serikali.

Amesema ni wazi kuwa jambo lolote la ndani la serikali au nyaraka zozote za serikali hazipaswi kusikika nje, ambapo kutokana na kuwepo kwa tabia ya kuvujisha taarifa hizo wakuu wa wilaya wanatakiwa kuchuka hatua mara moja, ili kukomesha tabia hiyo.

Hayo yamesemwa waziri mkuu MAJALIWA wakatia Akizindua Program ya Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi, kutoka katika Mkoa 6 hapa nchini ambayo yanayotolewa na Taasisi  ya Uongozi.

Hata hivyo Waziri Mkuu amesema kuwa katika kipindi hiki cha utandawazi suala la utunzaji wa taarifa za serikali bila kuvuja pamoja na matumzi mazuri ya nyaraka ni muhimu kuzingatiwa.

Akizungumza kwa niaba ya wakuu wa wilaya za mikoa 6 walioshiriki katika mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Dodoma CHRISTINA MDEME, amesema kuwa wao kama viongozi wako tayari kufanya kazi wakati wowote iwe usiku, mchana, kiangazi au masika bila kujali mazingira ya kazi.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu