Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema ili taifa liweze kuwa na watu waadilifu na wachapakazi, ni muhimu kwa wazazi kuhakikisha wanalifanyia kazi jukumu la kulea watoto kwenye misingi ya kumcha Mungu na muda mwingine kuhoji watoto kuhusu utajiri wanaoupata ghafla.

In Kitaifa
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema ili taifa liweze kuwa na watu waadilifu na wachapakazi, ni muhimu kwa wazazi kuhakikisha wanalifanyia kazi jukumu la kulea watoto kwenye misingi ya kumcha Mungu na muda mwingine kuhoji watoto kuhusu utajiri wanaoupata ghafla.
Majaliwa amesema kuwa Taifa la watu waadilifu na wachapakazi huanzia katika ngazi ya familia,  na  Kama kaya  haziishi kwa uadilifu, ni vigumu sana kuwa na taifa lenye wananchi waadilifu.
Waziri Mkuu ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wageni ,waliohudhuria harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa na nyumba ya Paroko katika Parokia teule ya Zuzu, nje kidogo ya mji wa Dodoma.
Harambee hiyo ilitanguliwa na ibada ya misa ya shukrani kwa ajili ya marehemu Mzee Xavery Mizengo Pinda, ambaye ni baba yake, Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda.
Mzee Xavery Pinda alifariki Novemba 27, mwaka jana katika hospitali ya mkoa wa Dodoma na kuzikwa kijijini kwake Kibaoni wilayani Mlele, Katavi.
Katika harambee hiyo, Waziri Mkuu na mke wake walichangia Sh milioni 10 ambapo jumla ya Sh milioni 160 zilikusanywa.
Kati ya hizo, Sh milioni 111.15 zilikuwa ni ahadi, Sh milioni 38.45 zilikuwa ni fedha taslimu na Sh milioni 10.403 zilikuwa ni thamani ya vifaa vya ujenzi vilivyotolewa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu