Waziri Mkuu wa DRC ajiuzulu kupisha uteuzi mwingine.

In Kimataifa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Samy Badibanga ametangaza kujiuzulu.

Hatua hii imekuja baada ya rais Joseph Kabila siku ya Jumanne, kulihotubia bunge na kuahidi kumteua Waziri Mkuu mpya ndani ya saa 48.

Badibanga mwenye umri wa miaka 54 aliteuliwa katika nafasi hiyo mwezi Novemba mwaka 2016 baada ya jitihada za kuwepo kwa mazungumzo ya kisiasa chini ya mjumbe wa Umoja wa Afrika.

Baada ya kutiwa saini kwa mkataba wa kisiasa kati ya serikal na upinzani mwisho wa mwezi Desemba mwaka 2016 baada ya upatanishi, wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki,ilikubaliwa kuwa Waziri Mkuu mpya ateuliwe kutoka upinzani.

Muda wa rais Kabila kukaa madarakani ulikamilika mwaka uliopita lakini kwa sababu ya mzozo wa kisiasa nchini humo, ameendelea kukaa madarakani baada ya Tume ya Uchaguzi kusema haina fedha za kuandaa Uchaguzi Mkuu.

Upinzani wamekuwa wakisema kuwa wanataka kupendekeza jina moja huku upande wa serikali ukisema kuwa upinzani kupendekeza majina matatu na rais kumteua mmoja.

Hata baada ya hotuba ya rais Kabila, wanasiasa wa upinzani wameonekana kutounga mkono na juhudi za rais Kabila kuwa Waziri Mkuu atapatikana baada ya  saa 48 na kupitisha uundwaji wa serikali ya mpito.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu