Waziri mkuu wa Japani wiki hii atazuru Urusi ambako atakua na mazungumzo na Rais vladmir Putin.

In Kimataifa

Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe wiki hii atazuru Urusi ambako atakuwa na mazungumzo na Rais Vladimir Putin mnamo wakati nchi hizo mbili zikijaribu kutafuta suluhisho la mzozo wa mipaka uliodumua kwa miaka mingi.

Ikulu ya Urusi, Kremlin, imesema hii leo kuwa mazungumzo ya viongozi hao yataangazia ushirikiano kati ya nchi hizo katika nyanja za kisiasa, biashara, uchumi na masuala ya kibinadamu.

Ziara hiyo inafuatia ziara ya Rais Putin nchini Japan mwezi Desemba mwaka jana ambayo ni ya kwanza katika kipindi cha miaka 11.

Hata hivyo, kwenye ziara hiyo ya Desemba, Putin na Abe walishindwa kupata ufumbuzi wa mzozo juu ya visiwa kadhaa, ambao umeyafanya mataifa hayo mawili hadi sasa kushindwa kusaini makubaliano rasmi ya kumalizika Vita vya Pili vya Dunia.

Siku hizo ikiitwa Jamhuri ya Muungano wa Kisovieti, Urusi ilivichukuwa visiwa kadhaa kaskazini mwa pwani ya Japan, mnamo mwaka 1945, wakati Vita hivyo vikikaribia ukingoni.

Tangu hapo, visiwa hivyo vimekuwa kiini cha mzozo mkubwa kati ya Urusi na Japan.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu