Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amewaacha mawaziri wake waandamizi katika nafasi zao wakati ameunda serikali mpya ya walio wachache akiungwa mkono na chama kidogo cha Ireland Kaskazini.

In Kimataifa
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amewaacha mawaziri wake waandamizi katika nafasi zao wakati ameunda serikali mpya ya walio wachache akiungwa mkono na chama kidogo cha Ireland Kaskazini.
Chama cha May cha Conservative kilipoteza wingi wa viti bungeni katika uchaguzi wa kitaifa uliofanyika siku ya Alhamis ambao chama cha upinzani cha Labour kilinyakua zaidi ya viti vipya 30.
May sasa ataongoza serikali pamoja na chama cha siasa za mrengo wa kulia cha Democratic Unionist – DUP, ambacho viti vyake 10 vitampa wingi wa viti kwa ajili ya kuongoza.
Waziri huyo Mkuu aliitisha uchaguzi wa mapema katika jaribio la kuiimarisha nafasi yake katika Umoja wa Ulaya wakati Uingereza ikijiandaa kujiondoa katika Umoja huo.
Badala yake, Mbunge wa Labour David Lemmy anahisi kuwa uchaguzi huo umedhoofisha mamlaka yake.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu