Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amewaacha mawaziri wake waandamizi katika nafasi zao wakati ameunda serikali mpya ya walio wachache akiungwa mkono na chama kidogo cha Ireland Kaskazini.

In Kimataifa
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amewaacha mawaziri wake waandamizi katika nafasi zao wakati ameunda serikali mpya ya walio wachache akiungwa mkono na chama kidogo cha Ireland Kaskazini.
Chama cha May cha Conservative kilipoteza wingi wa viti bungeni katika uchaguzi wa kitaifa uliofanyika siku ya Alhamis ambao chama cha upinzani cha Labour kilinyakua zaidi ya viti vipya 30.
May sasa ataongoza serikali pamoja na chama cha siasa za mrengo wa kulia cha Democratic Unionist – DUP, ambacho viti vyake 10 vitampa wingi wa viti kwa ajili ya kuongoza.
Waziri huyo Mkuu aliitisha uchaguzi wa mapema katika jaribio la kuiimarisha nafasi yake katika Umoja wa Ulaya wakati Uingereza ikijiandaa kujiondoa katika Umoja huo.
Badala yake, Mbunge wa Labour David Lemmy anahisi kuwa uchaguzi huo umedhoofisha mamlaka yake.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu