Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amewasili nchini Japan.

In Kimataifa

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amewasili nchini Japan kwa ziara rasmi, akilenga kutuliza wasiwasi kuhusu hatua ya Uingereza kujiondoa katika Umoja wa Ulaya na kuanzisha mazungumzo ya mapema kuhusu biashara huria na taifa hilo la tatu kiuchumi duniani.

May anatarajiwa kukutana na mwenyekiti wa kampuni ya kutengeneza magari ya Toyota wakati wa ziara yake hiyo ya siku tatu ambayo inaanzia mjini Osaka kabla ya kuelekea Tokyo ambako atakutana na Mfalme Akihito na Waziri Mkuu Shinzo Abe.

Hatua ya Uingereza kujiondoa katika Umoja wa Ulaya ilizusha wasiwasi nchini Japan kuhusu athari za hatua hiyo kwa kampuni zenye maslahi makubwa ya kibiashara nchini humo.

Afisa wa wizara ya Mambo ya Kigeni ya Japan anayehusika na masuala ya Umoja wa Ulaya alisema kabla ya ziara ya May kuwa watataka uwazi na uhakika kutoka kwa Uingereza ili kupunguza athari zinazoweza kutokea kwa kampuni za Japan.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu