Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amewasili nchini Japan.

In Kimataifa

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amewasili nchini Japan kwa ziara rasmi, akilenga kutuliza wasiwasi kuhusu hatua ya Uingereza kujiondoa katika Umoja wa Ulaya na kuanzisha mazungumzo ya mapema kuhusu biashara huria na taifa hilo la tatu kiuchumi duniani.

May anatarajiwa kukutana na mwenyekiti wa kampuni ya kutengeneza magari ya Toyota wakati wa ziara yake hiyo ya siku tatu ambayo inaanzia mjini Osaka kabla ya kuelekea Tokyo ambako atakutana na Mfalme Akihito na Waziri Mkuu Shinzo Abe.

Hatua ya Uingereza kujiondoa katika Umoja wa Ulaya ilizusha wasiwasi nchini Japan kuhusu athari za hatua hiyo kwa kampuni zenye maslahi makubwa ya kibiashara nchini humo.

Afisa wa wizara ya Mambo ya Kigeni ya Japan anayehusika na masuala ya Umoja wa Ulaya alisema kabla ya ziara ya May kuwa watataka uwazi na uhakika kutoka kwa Uingereza ili kupunguza athari zinazoweza kutokea kwa kampuni za Japan.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu