Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed amesema sasa ni wakati muafaka kwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB) kuwekeza Visiwani Zanzibar ili kuchagiza juhudi za Serikali za kuwawezesha kiuchumi wakazi wa visiwa hivyo wanaojishughulisha na sekta za kilimo, uvuvi na uchakataji mazao.

In Kitaifa

Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed amesema sasa ni wakati muafaka kwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB) kuwekeza Visiwani Zanzibar ili kuchagiza juhudi za Serikali za kuwawezesha kiuchumi wakazi wa visiwa hivyo wanaojishughulisha na sekta za kilimo, uvuvi na uchakataji mazao.

Mhe. Hamad amesema Visiwa vya Zanzibar vina maeneo mengi ya uwekezaji yenye kuweza kuongeza tija na ongezeko la uchumi visiwani humo ikiwa kutakuwa na uwekezaji mkubwa katika maeneo hayo.

Kwa mujibu wa Mhe. Waziri, Zanzibar ni miongoni mwa visiwa vyenye utajiri mkubwa ambavyo kukiwa na uwekezaji wa kimkakati vinaweza kutokea matokeo makubwa na yenye kuwanufaisha wananchi wengi.

Akizungumza na Mhe. Waziri, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga amesema Serikali iliamua kuanzisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ili kusaidia kukabiliana na mapungufu ya wakulima nchini kote ili kuhuisha upatikanaji wa mikopo katika sekta ya kilimo na kuchagiza mapinduzi katika  kilimo nchini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu