Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani afanya ziara ya ghafla nchini Somalia.

In Kimataifa
 Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Sigmar Gabriel, amefanya ziara ya ghafla nchini Somalia, ambako ameahidi kuongeza mara mbili msaada wa nchi yake kwa taifa hilo lililoathiriwa vibaya, na ukame katika Pembe ya Afrika.
Gabriel amewasili mjini Mogadishu jana kukiwa na ulinzi mkali, na hiyo ikiwa ziara ya kwanza ya waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani nchini Somalia.
Waziri huyo ameonya kuwa miaka kadhaa ya ukame inasababisha janga la kibinaadamu ,ambalo linahitaji msaada mkubwa kutoka nje.
Tayari, Ujerumani ilikuwa imeshaahidi msaada wa dola milioni 76 kwa Somalia, ambako zaidi ya watu milioni sita wanauhitaji mkubwa wa msaada wa kiutu.
Katika mkutano wake na Waziri Mkuu wa Somalia, Hassan Ali Khaire, Sigmar Gabriel amesema Ujerumani iko tayari kuongeza maradufu msaada huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu