Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani afanya ziara ya ghafla nchini Somalia.

In Kimataifa
 Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Sigmar Gabriel, amefanya ziara ya ghafla nchini Somalia, ambako ameahidi kuongeza mara mbili msaada wa nchi yake kwa taifa hilo lililoathiriwa vibaya, na ukame katika Pembe ya Afrika.
Gabriel amewasili mjini Mogadishu jana kukiwa na ulinzi mkali, na hiyo ikiwa ziara ya kwanza ya waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani nchini Somalia.
Waziri huyo ameonya kuwa miaka kadhaa ya ukame inasababisha janga la kibinaadamu ,ambalo linahitaji msaada mkubwa kutoka nje.
Tayari, Ujerumani ilikuwa imeshaahidi msaada wa dola milioni 76 kwa Somalia, ambako zaidi ya watu milioni sita wanauhitaji mkubwa wa msaada wa kiutu.
Katika mkutano wake na Waziri Mkuu wa Somalia, Hassan Ali Khaire, Sigmar Gabriel amesema Ujerumani iko tayari kuongeza maradufu msaada huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu