Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amesema uchumi wa nchi ukitengemaa, serikali itaongeza posho za madiwani na watendaji wa vijiji.

In Kitaifa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amesema uchumi wa nchi ukitengemaa, serikali itaongeza posho za madiwani na watendaji wa vijiji.

Simbachawene amesema hayo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema).

Nassari alikuwa ametaka kusikia serikali itaongeza lini posho ya watendaji hao ambapo Simbachawene amesema, Serikali inatambua mchango wa viongozi hao katika maendeleo ya nchi, lakini kutokana na uchumi kutotengemaa, haiwezi kuwaongeza posho.

Akijibu swali la Mbunge wa Musoma Mjini, Vedasto Manyinyi (CCM), Naibu Waziri wa Nchi, ofisi ya Rais (Tamesemi), Seleman Jafo alisema serikali inatambua mchango wao katika kusimamia shughuli za maendeleo. Katika swali lake la msingi, Manyinyi alitaka kujua kama serikali imeridhika na malipo ya wenyeviti wa mitaa na madiwani hao.

Jafo amesema majukumu yanayotekelezwa na viongozi hao ni utekelezaji wa dhana na ugatuaji wa madaraka, kwa wananchi ambapo mipango yote uamuzi unafanyika katika ngazi za msingi wa serikali za mtaa.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu