Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amesema uchumi wa nchi ukitengemaa, serikali itaongeza posho za madiwani na watendaji wa vijiji.

In Kitaifa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amesema uchumi wa nchi ukitengemaa, serikali itaongeza posho za madiwani na watendaji wa vijiji.

Simbachawene amesema hayo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema).

Nassari alikuwa ametaka kusikia serikali itaongeza lini posho ya watendaji hao ambapo Simbachawene amesema, Serikali inatambua mchango wa viongozi hao katika maendeleo ya nchi, lakini kutokana na uchumi kutotengemaa, haiwezi kuwaongeza posho.

Akijibu swali la Mbunge wa Musoma Mjini, Vedasto Manyinyi (CCM), Naibu Waziri wa Nchi, ofisi ya Rais (Tamesemi), Seleman Jafo alisema serikali inatambua mchango wao katika kusimamia shughuli za maendeleo. Katika swali lake la msingi, Manyinyi alitaka kujua kama serikali imeridhika na malipo ya wenyeviti wa mitaa na madiwani hao.

Jafo amesema majukumu yanayotekelezwa na viongozi hao ni utekelezaji wa dhana na ugatuaji wa madaraka, kwa wananchi ambapo mipango yote uamuzi unafanyika katika ngazi za msingi wa serikali za mtaa.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu