Waziri wa Uganda ajeruhiwa na mwanae kufa baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana

Watu wenye silaha wamemshambulia na kumjeruhi Waziri na Kamanda wa zamani wa jeshi la Uganda, na kumuua binti yake na dereva.

Walioshuhudia tukio hilo wanasema washambuliaji ambao hawajafahamika walliokuwa kwenye pikipiki walifyatua risasi kadhaa kwenye gari alimokuwa Jenerali Katumba Wamala.

Shambulio hilo limeonekana kama jaribio la kumuua kamanda huyo wa zamani wa jeshi na Mkuu wa zamani wa polisi ambaye kwa sasa ni Waziri wa Ujenzi na Uchuku na limemewashtua wengi nchini Uganda.

Kuna takriban mashimo saba ya risasi kwenye dirisha la gari la Jenerali Katumba Wamala. Binti yake na dereva wote wameuawa.

Washambuliaji walitoroka kwa pikipiki zao baada ya kutekeleza shambulio hilo.

Picha ya video kutoka kwenye eneo la tukio inamuonesha Jenerali Wamala huku nguo zake zikiwa zimejaa damu –akibebwa kwenye pikipiki na kukimbizwa hospitalini.

Shambulio hili dhidi ya mmoja wa wanasiasa na wanajeshi wanaoheshimika zaidi nchini Uganda pia linawakumbusha wengi mauaji ya watu maarufu waliouawa miaka ya nyuma kwa risasi.

Katika miaka ya hivi karibuni mashambulio sawa na shambulio hili ni pamoja na hakimu, viongozi wa Kiislamu , mshirika maarufu wa kisasa wa Rais Yoweri Museveni na Mkuu wa ngazi ya juu wa polisi.

Wahusika wa mauaji hayo hawajawahi kushitakiwa.

Exit mobile version