Waziri wa ulinzi wa Marekani aitaka Ufaransa kuendelea kupambana na ugaidi barani Africa.

In Kimataifa

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Jim Mattis ameitaka Ufaransa kuendelea kupambana na ugaidi barani Afrika. Mattis ametoa wito huo baada ya ziara yake nchini Djibouti, eneo ambalo ni la mkakati wa jeshi la Marekani kwa bara la Afrika.

Aidha, amesema kuwa Marekani inaunga mkono Ufaransa katika vita dhidi ya magaidi katika eneo la Sahel hasa nchini Mauritania, Mali, Chad, Niger na Burkina Faso.

Waziri wa Ulinzi wa Marekani James Mattis allimuelezea rais wa Djibouti Ismail Omar Guelleh, wasiwasi wa Marekani kuhusu ujenzi wa kambi ya kwanza ya kijeshi ya China nje ya nchi, karibu na kambi ya Lemonnier ya jeshi la Marekani barani Afrika.

Marekani ina kambi moja peke barani Afrika ambayo imejengwa nchini Djibouti, na ina askari 4,000 kwa mujibu wa Pentagon.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu