Waziri wa ulinzi wa Marekani aitaka Ufaransa kuendelea kupambana na ugaidi barani Africa.

In Kimataifa

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Jim Mattis ameitaka Ufaransa kuendelea kupambana na ugaidi barani Afrika. Mattis ametoa wito huo baada ya ziara yake nchini Djibouti, eneo ambalo ni la mkakati wa jeshi la Marekani kwa bara la Afrika.

Aidha, amesema kuwa Marekani inaunga mkono Ufaransa katika vita dhidi ya magaidi katika eneo la Sahel hasa nchini Mauritania, Mali, Chad, Niger na Burkina Faso.

Waziri wa Ulinzi wa Marekani James Mattis allimuelezea rais wa Djibouti Ismail Omar Guelleh, wasiwasi wa Marekani kuhusu ujenzi wa kambi ya kwanza ya kijeshi ya China nje ya nchi, karibu na kambi ya Lemonnier ya jeshi la Marekani barani Afrika.

Marekani ina kambi moja peke barani Afrika ambayo imejengwa nchini Djibouti, na ina askari 4,000 kwa mujibu wa Pentagon.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu