Waziri wa ulinzi wa Marekani awasili Djibuti kwa ziara fupi.

In Kimataifa

Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Jim Mattis, amewasili Djibuti kwa ziara fupi, katika taifa la kimkakati la Pembe ya Afrika. Pia ni taifa pekee katika bara hilo lenye kambi ya kijeshi ya kudumu ya Marekani.

Kambi ya Lemonnier, iliyo na wanajeshi 4,000 wa Kimarekani na makandarasi ni muhimu kwa operesheni za kijeshi za Marekani inazozifanya nchini Somalia dhidi ya makundi ya wanamgambo kama vile al-Shabbab.

Kambi hiyo pia inasaidia operesheni za kijeshi za Marekani za nchini Yemen, ambapo vikosi maalumu vinafanya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani ya mara kwa mara dhidi ya kundi la Al-Qaeda, katika Rasi ya Uarabuni.

Mattis anatarajiwa kukutana na rais wa Djibuti, Ismail Omar Gue lleh pamoja na Jenerali Thomas Waldha user, kamanda wa vikosi vya Marekani vilivyopo barani Afrika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu