Waziri wa ulinzi wa Marekani awasili Djibuti kwa ziara fupi.

In Kimataifa

Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Jim Mattis, amewasili Djibuti kwa ziara fupi, katika taifa la kimkakati la Pembe ya Afrika. Pia ni taifa pekee katika bara hilo lenye kambi ya kijeshi ya kudumu ya Marekani.

Kambi ya Lemonnier, iliyo na wanajeshi 4,000 wa Kimarekani na makandarasi ni muhimu kwa operesheni za kijeshi za Marekani inazozifanya nchini Somalia dhidi ya makundi ya wanamgambo kama vile al-Shabbab.

Kambi hiyo pia inasaidia operesheni za kijeshi za Marekani za nchini Yemen, ambapo vikosi maalumu vinafanya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani ya mara kwa mara dhidi ya kundi la Al-Qaeda, katika Rasi ya Uarabuni.

Mattis anatarajiwa kukutana na rais wa Djibuti, Ismail Omar Gue lleh pamoja na Jenerali Thomas Waldha user, kamanda wa vikosi vya Marekani vilivyopo barani Afrika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu