Wenger awatupia lawama waamuzi Uingereza.

In Kimataifa, Michezo

Kocha wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger ametoa lawama kwa waamuzi kwa kusema viwango vya usimamizi wa mechi katika ligi kuu ya Uingereza vimeendelea kudorora mwaka baada ya mwaka.

Lawama za Wenger zinakuja baada kipigo cha mabao 3-1 ambacho Arsenal walipata jana kutoka kwa Manchester City katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa kwenye uwanja wa Etihad.

Wenger anaamini mshambuliaji wa Man City Raheem Sterling alijiangusha na kupewa penati iliyopigwa na Sergio Aguero dakika ya 50 ambayo iliwasaidia wenyeji kupata bao la pili.

”Nafikiri waamuzi hawafanyi kazi ya kutosha amesema, viwango vinashuka kila msimu kwa sasa na kwa jumla haikubaliki,” alisema Wenger.

City walipata bao la tatu lililofungwa na Gabriel Jesus dakika ya 74 lakini Wenger anaamini bao hilo halikufaa kukubaliwa kwani lilikuwa la kuotea.

Matokeo hayo yameifanya Manchester City kuzidi kujikita kileleni mwa EPL wakiwa na pointi 11 huku Arsenal wakiwa na katika nafasi ya 6 wakiwa na pointi 19 baada ya kucheza michezo 11.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu