Wenger awatupia lawama waamuzi Uingereza.

In Kimataifa, Michezo

Kocha wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger ametoa lawama kwa waamuzi kwa kusema viwango vya usimamizi wa mechi katika ligi kuu ya Uingereza vimeendelea kudorora mwaka baada ya mwaka.

Lawama za Wenger zinakuja baada kipigo cha mabao 3-1 ambacho Arsenal walipata jana kutoka kwa Manchester City katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa kwenye uwanja wa Etihad.

Wenger anaamini mshambuliaji wa Man City Raheem Sterling alijiangusha na kupewa penati iliyopigwa na Sergio Aguero dakika ya 50 ambayo iliwasaidia wenyeji kupata bao la pili.

”Nafikiri waamuzi hawafanyi kazi ya kutosha amesema, viwango vinashuka kila msimu kwa sasa na kwa jumla haikubaliki,” alisema Wenger.

City walipata bao la tatu lililofungwa na Gabriel Jesus dakika ya 74 lakini Wenger anaamini bao hilo halikufaa kukubaliwa kwani lilikuwa la kuotea.

Matokeo hayo yameifanya Manchester City kuzidi kujikita kileleni mwa EPL wakiwa na pointi 11 huku Arsenal wakiwa na katika nafasi ya 6 wakiwa na pointi 19 baada ya kucheza michezo 11.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu