Wenyeviti wa CCWT washinikiza uchaguzi ufanyike katika chama chao.

In Kitaifa

Baadhi ya Wenyeviti wa Chama cha Wafugaji  nchini (CCWT) ambao wanatoka katika Kanda saba za kifugaji nchini,wanatarajia kwenda kwa Msajili wa  Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi wa vyama vya ushirika, kwa lengo la kushinikiza uchaguzi wa viongozi ufanyike katika Chama chao.

Hatua ya Wenyeviti hao kwenda kwa Msajili huyo wa Vyama inatokana na wao kutokuwa na imani na uongozi wa sasa ambao ni wa mpito, na wanadai kuwa umekuwa ukikiendesha Chama hicho kidiktekta licha ya muda wao wa kuwa madarakani kwisha.

Kauli hiyo imetolewa leo Mjini Dodoma na Wenyeviti hao wakati wakizungumza na waandishi wa habari baada ya kutofautiana katika mkutano mkuu wa wafugaji.

Mmoja wa Wenyeviti hao,WAMARWA KUSUNDA amesema kuwa waliuchagua uongozi wa mpito ambao ni mwenyekiti,katibu mkuu,mtunza hazina pamoja na wajumbe 12 wa kamati tendaji mnamo mwaka 2015 kwa lengo la kutetea maslahi ya wafugaji.

Hata hivyo amesema kuwa Serikali kupitia Mkamu wa Rais Samia Suluhu Hassan aliwaagiza Wakuu wa wilaya nchini, kwa kushirikiana na viongozi wa wafugaji kutenga maeneo ya malisho lakini suala hilo halijatekelezwa na badala yake Uongozi huo, unataka kwenda kwa makamu wa rais kulalamikia kuwa maeneo hayajatengwa jambo ambalo ni kutaka kuwachonganisha na wakuu hao wa wilaya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu