Wenyeviti wa CCWT washinikiza uchaguzi ufanyike katika chama chao.

In Kitaifa

Baadhi ya Wenyeviti wa Chama cha Wafugaji  nchini (CCWT) ambao wanatoka katika Kanda saba za kifugaji nchini,wanatarajia kwenda kwa Msajili wa  Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi wa vyama vya ushirika, kwa lengo la kushinikiza uchaguzi wa viongozi ufanyike katika Chama chao.

Hatua ya Wenyeviti hao kwenda kwa Msajili huyo wa Vyama inatokana na wao kutokuwa na imani na uongozi wa sasa ambao ni wa mpito, na wanadai kuwa umekuwa ukikiendesha Chama hicho kidiktekta licha ya muda wao wa kuwa madarakani kwisha.

Kauli hiyo imetolewa leo Mjini Dodoma na Wenyeviti hao wakati wakizungumza na waandishi wa habari baada ya kutofautiana katika mkutano mkuu wa wafugaji.

Mmoja wa Wenyeviti hao,WAMARWA KUSUNDA amesema kuwa waliuchagua uongozi wa mpito ambao ni mwenyekiti,katibu mkuu,mtunza hazina pamoja na wajumbe 12 wa kamati tendaji mnamo mwaka 2015 kwa lengo la kutetea maslahi ya wafugaji.

Hata hivyo amesema kuwa Serikali kupitia Mkamu wa Rais Samia Suluhu Hassan aliwaagiza Wakuu wa wilaya nchini, kwa kushirikiana na viongozi wa wafugaji kutenga maeneo ya malisho lakini suala hilo halijatekelezwa na badala yake Uongozi huo, unataka kwenda kwa makamu wa rais kulalamikia kuwa maeneo hayajatengwa jambo ambalo ni kutaka kuwachonganisha na wakuu hao wa wilaya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu