Wito watolewa na Waziri wa Mambo ya nje wa China kuziondoa silaha za kinyuklia katika rasi ya korea.

In Kimataifa

Waziri wa mambo ya nje wa China ametoa wito wa kuondoa silaha za kinyuklia katika rasi ya Korea, huku mvutano juu ya mipango ya makombora na silaha za kinyuklia ya Korea Kaskazini ukiwa unazidi kupamba moto.

Wang Yi amewaambia maripota wa mjini Athens baada ya kukutana na mwenzake wa Ugiriki, Nikos Kotzias, kwamba China inaunga mkono kikamilifu kuondolewa kwa silaha zozote za kinyuklia katika eneo hilo, ili kupatikane utulivu na amani.

Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka China kuchukua hatua imara, kuishinikiza Korea Kaskazini kusitisha mipango yake ya kinyuklia na makombora ya masafa marefu.

Katika wiki za hivi karibuni, Korea Kaskazini imekuwa ikitishia kujibu mashambulizi yoyote ya uchokozi.

Aidha shirika la habari la Yonhap la taifa hilo, limeripoti leo hii kwamba raia mmoja wa Kimarekani amekamatwa akiwa anajaribu kuikimbia Korea Kaskazini.

Ni raia wa tatu wa Kimarekani kushikiliwa nchini humo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu