WIZARA ya Nishati na Madini imesisitiza kuwa itaendelea kutumia watalaamu, kupata ushauri wa maeneo yanayohitaji kufanyiwa utafiti wa mafuta na gesi ,na haitaliacha suala hilo liingiliwe kisiasa.

In Kitaifa

WIZARA ya Nishati na Madini imesisitiza kuwa itaendelea kutumia watalaamu, kupata ushauri wa maeneo yanayohitaji kufanyiwa utafiti wa mafuta na gesi ,na haitaliacha suala hilo liingiliwe kisiasa.

Msimamo huo umetolewa bungeni Dodoma jana na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo  wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa viti maalum, Susan Lyimo (Chadema).

Lyimo ametaka kujua ni kwanini serikali haimtumii mzee maarufu katika mji wa Mlimba, anayedaiwa kuwa na taarifa kamili kuhusu uwepo wa mafuta kwenye bwawa lililopo mjini hapo, ili lifanyiwe utafiti.

Akijibu maswali hayo, Profesa Muhongo amesema serikali haiwezi kwenda kwa mzee yeyote kuuliza taarifa za utafiti wa mafuta na gesi ,kwa kuwa suala hilo ni la kitaaluma zaidi na utafiti wake hufanyika baada ya wataalam kuwa na uhakika, wa uwezekano wa kupatikana kwa nishati hizo

Aidha amesema katika utafutaji wa mafuta duniani, wakati mwingine utafiti huonesha kuwepo au ukosefu wa nishati hiyo, na kwa sasa Tanzania ina mpango wa kubadilisha mbinu ya utafutaji wa mafuta hayo.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu