WIZARA ya Nishati na Madini imesisitiza kuwa itaendelea kutumia watalaamu, kupata ushauri wa maeneo yanayohitaji kufanyiwa utafiti wa mafuta na gesi ,na haitaliacha suala hilo liingiliwe kisiasa.

In Kitaifa

WIZARA ya Nishati na Madini imesisitiza kuwa itaendelea kutumia watalaamu, kupata ushauri wa maeneo yanayohitaji kufanyiwa utafiti wa mafuta na gesi ,na haitaliacha suala hilo liingiliwe kisiasa.

Msimamo huo umetolewa bungeni Dodoma jana na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo  wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa viti maalum, Susan Lyimo (Chadema).

Lyimo ametaka kujua ni kwanini serikali haimtumii mzee maarufu katika mji wa Mlimba, anayedaiwa kuwa na taarifa kamili kuhusu uwepo wa mafuta kwenye bwawa lililopo mjini hapo, ili lifanyiwe utafiti.

Akijibu maswali hayo, Profesa Muhongo amesema serikali haiwezi kwenda kwa mzee yeyote kuuliza taarifa za utafiti wa mafuta na gesi ,kwa kuwa suala hilo ni la kitaaluma zaidi na utafiti wake hufanyika baada ya wataalam kuwa na uhakika, wa uwezekano wa kupatikana kwa nishati hizo

Aidha amesema katika utafutaji wa mafuta duniani, wakati mwingine utafiti huonesha kuwepo au ukosefu wa nishati hiyo, na kwa sasa Tanzania ina mpango wa kubadilisha mbinu ya utafutaji wa mafuta hayo.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu