WIZARA ya Nishati na Madini imesisitiza kuwa itaendelea kutumia watalaamu, kupata ushauri wa maeneo yanayohitaji kufanyiwa utafiti wa mafuta na gesi ,na haitaliacha suala hilo liingiliwe kisiasa.

In Kitaifa

WIZARA ya Nishati na Madini imesisitiza kuwa itaendelea kutumia watalaamu, kupata ushauri wa maeneo yanayohitaji kufanyiwa utafiti wa mafuta na gesi ,na haitaliacha suala hilo liingiliwe kisiasa.

Msimamo huo umetolewa bungeni Dodoma jana na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo  wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa viti maalum, Susan Lyimo (Chadema).

Lyimo ametaka kujua ni kwanini serikali haimtumii mzee maarufu katika mji wa Mlimba, anayedaiwa kuwa na taarifa kamili kuhusu uwepo wa mafuta kwenye bwawa lililopo mjini hapo, ili lifanyiwe utafiti.

Akijibu maswali hayo, Profesa Muhongo amesema serikali haiwezi kwenda kwa mzee yeyote kuuliza taarifa za utafiti wa mafuta na gesi ,kwa kuwa suala hilo ni la kitaaluma zaidi na utafiti wake hufanyika baada ya wataalam kuwa na uhakika, wa uwezekano wa kupatikana kwa nishati hizo

Aidha amesema katika utafutaji wa mafuta duniani, wakati mwingine utafiti huonesha kuwepo au ukosefu wa nishati hiyo, na kwa sasa Tanzania ina mpango wa kubadilisha mbinu ya utafutaji wa mafuta hayo.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu