Wizara ya ulinzi nchini Kenya imeshutumu taarifa zilizokuwa zimeenezwa kwamba msemaji wa jeshi la Kenya Kanali Joseph Owuoth alikuwa ametoweka.

In Kimataifa

Wizara ya ulinzi nchini Kenya imeshutumu taarifa zilizokuwa zimeenezwa kwamba msemaji wa jeshi la Kenya Kanali Joseph Owuoth alikuwa ametoweka.

Waziri Raychelle Omamo, akihutubia wanahabari, amesema taarifa kama hizo zinatishia usalama na kuzua wasiwasi miongoni mwa maafisa wa jeshi na familia zao.

Kanali Owuoth aligonga vichwa vya habari baada ya kuthibitisha kwamba nyaraka zilizokuwa zimetumiwa na muungano wa upinzani nchini humo Nasa kudai kwamba serikali inapanga kutumia jeshi kutekeleza ‘mapinduzi’ ili kuendelea kusalia madarakani zilikuwa halisi.

Msemaji huyo hata hivyo alisema nyaraka hizo zilinukuliwa na kufasiriwa visivyo.

Bi Omamo, kwenye kikao hicho, alisema baada ya uchunguzi, imebainika kwamba nyaraka hizo zilizotumiwa na muungano wa Nasa zilikuwa ghush.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu