Zaidi ya Milioni 200 zimepatikana kutoka kwa wadau mbalimbali wanaoendelea kuchangia rambirambi kwa familia za wanafunzi 32, wa shule ya Lucky Vincent waliopoteza maisha kwenye ajali ya basi iliyotokea wiki iliyopita

In Kitaifa

Zaidi  ya  Milioni 200 zimepatikana kutoka kwa wadau mbalimbali wanaoendelea  kuchangia  rambirambi kwa familia za wanafunzi 32, wa shule ya Lucky Vincent waliopoteza maisha kwenye ajali ya basi iliyotokea wiki iliyopita.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa  habari  ofisini kwake ,Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo,amesema kuwa hadi sasa wamepokea kiasi cha Sh Milioni 215, kutoka kwa wadau mbalimbali ikiwemo Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Gambo amewataja wadau wengine kuwa ni Baraza la Wawakilishi
Zanzibar,Wizara ya Elimu Zanzibar,mifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii pamoja na wadau wengine.
Amesema mpaka sasa zaidi ya Sh Milioni 190 zimetumika ikiwemo Sh Milioni 3,laki nane na elfu hamsini 850,000, kwa familia 32 zilizopoteza watoto wao katika ajali hiyo,gharama za mazishi ikiwemo magari na usafiri kwa ajili ya maziko yaliyofanyika katika mikoa ya Arusha,Iringa,Tanga,Mbeya na Kilimanjaro

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu