Zaidi ya Milioni 200 zimepatikana kutoka kwa wadau mbalimbali wanaoendelea kuchangia rambirambi kwa familia za wanafunzi 32, wa shule ya Lucky Vincent waliopoteza maisha kwenye ajali ya basi iliyotokea wiki iliyopita

In Kitaifa

Zaidi  ya  Milioni 200 zimepatikana kutoka kwa wadau mbalimbali wanaoendelea  kuchangia  rambirambi kwa familia za wanafunzi 32, wa shule ya Lucky Vincent waliopoteza maisha kwenye ajali ya basi iliyotokea wiki iliyopita.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa  habari  ofisini kwake ,Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo,amesema kuwa hadi sasa wamepokea kiasi cha Sh Milioni 215, kutoka kwa wadau mbalimbali ikiwemo Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Gambo amewataja wadau wengine kuwa ni Baraza la Wawakilishi
Zanzibar,Wizara ya Elimu Zanzibar,mifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii pamoja na wadau wengine.
Amesema mpaka sasa zaidi ya Sh Milioni 190 zimetumika ikiwemo Sh Milioni 3,laki nane na elfu hamsini 850,000, kwa familia 32 zilizopoteza watoto wao katika ajali hiyo,gharama za mazishi ikiwemo magari na usafiri kwa ajili ya maziko yaliyofanyika katika mikoa ya Arusha,Iringa,Tanga,Mbeya na Kilimanjaro

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu