Zaidi ya watu 14 wameuawa nchini Somalia baada ya makabiliano kuzuka kati ya wanajeshi na raia kuhusiana na msaada wa chakula.

In Kimataifa
Zaidi ya watu 14 wameuawa nchini Somalia baada ya makabiliano kuzuka kati ya wanajeshi na raia kuhusiana na msaada wa chakula.
 Maafisa wanasema wengi wa waliokufa ni raia ambao walijikuta katikati ya vurugu hizo kati ya makundi mawili ya wanajeshi, ambapo baadhi yao walijaribu kuiba magunia ya chakula kilichostahili kupewa watu waliopoteza makaazi.
Makabiliano hayo yalitokea katika mji wa kusini magharibi wa Baidoa, ambao umeshuhudia mmiminiko wa maelfu ya watu kufuatia hali mbaya zaidi ya ukame kuwahi kutokea katika zaidi ya miaka 70.
Somalia ni moja kati ya nchi nne zilizochaguliwa na Umoja wa Mataifa katika mpango wa ombi la msaada wa dola bilioni 4.4 ili kuepusha janga la njaa pamoja na Nigeria, Sudan Kusini na Yemen

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu