Zaidi ya watu 14 wameuawa nchini Somalia baada ya makabiliano kuzuka kati ya wanajeshi na raia kuhusiana na msaada wa chakula.

In Kimataifa
Zaidi ya watu 14 wameuawa nchini Somalia baada ya makabiliano kuzuka kati ya wanajeshi na raia kuhusiana na msaada wa chakula.
 Maafisa wanasema wengi wa waliokufa ni raia ambao walijikuta katikati ya vurugu hizo kati ya makundi mawili ya wanajeshi, ambapo baadhi yao walijaribu kuiba magunia ya chakula kilichostahili kupewa watu waliopoteza makaazi.
Makabiliano hayo yalitokea katika mji wa kusini magharibi wa Baidoa, ambao umeshuhudia mmiminiko wa maelfu ya watu kufuatia hali mbaya zaidi ya ukame kuwahi kutokea katika zaidi ya miaka 70.
Somalia ni moja kati ya nchi nne zilizochaguliwa na Umoja wa Mataifa katika mpango wa ombi la msaada wa dola bilioni 4.4 ili kuepusha janga la njaa pamoja na Nigeria, Sudan Kusini na Yemen

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu