Zambia: Jeshi la polisi limemtia mbaroni kiongozi wa chama kidogo cha upinzani.

In Kimataifa

Jeshi la polisi nchini Zambia hapo jana limemtia mbaroni kiongozi wa chama kidogo cha upinzani nchini humo cha United Progressive Party ambaye ni mkosoaji wa Rais Edgar Lungu.

Kukamatwa kwa mwanasiasa huyo ni hatua ya hivi karibuni dhidi ya wapinzani wa kisiasa nchini Zambia.

Savior Chishimba ambaye ni kiongozi wa chama cha United Progressive Party alikamatwa na maafisa wa polisi baada ya kuonekana katika mahojiano kwenye kituo kimoja cha televisheni ya binafsi mjini Lusaka.

Rais wa Zambia Edgar Lungu mwezi uliopita alitangaza kuchukua hatua zaidi za kiusalama ambazo zinalipa mamlaka zaidi jeshi la polisi kuwatia mbaroni watu huku pia kiongozi huyo akivishutumu vyama vya upinzani nchini humo kwa kuhusika na vitendo vya vurugu.

Hakainde Hichilema kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Zambia cha United Party for National Development amekuwa gerezani tangu mwezi April.

Rais Egar Lungu amekuwa akikanusha madai kuwa anajaribu kuunda utawala wa kiimla na anawashutumu mahasimu wake kisiasa kwa kutaka kubadilisha matokeo ya uchaguzi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu