Zambia: Jeshi la polisi limemtia mbaroni kiongozi wa chama kidogo cha upinzani.

In Kimataifa

Jeshi la polisi nchini Zambia hapo jana limemtia mbaroni kiongozi wa chama kidogo cha upinzani nchini humo cha United Progressive Party ambaye ni mkosoaji wa Rais Edgar Lungu.

Kukamatwa kwa mwanasiasa huyo ni hatua ya hivi karibuni dhidi ya wapinzani wa kisiasa nchini Zambia.

Savior Chishimba ambaye ni kiongozi wa chama cha United Progressive Party alikamatwa na maafisa wa polisi baada ya kuonekana katika mahojiano kwenye kituo kimoja cha televisheni ya binafsi mjini Lusaka.

Rais wa Zambia Edgar Lungu mwezi uliopita alitangaza kuchukua hatua zaidi za kiusalama ambazo zinalipa mamlaka zaidi jeshi la polisi kuwatia mbaroni watu huku pia kiongozi huyo akivishutumu vyama vya upinzani nchini humo kwa kuhusika na vitendo vya vurugu.

Hakainde Hichilema kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Zambia cha United Party for National Development amekuwa gerezani tangu mwezi April.

Rais Egar Lungu amekuwa akikanusha madai kuwa anajaribu kuunda utawala wa kiimla na anawashutumu mahasimu wake kisiasa kwa kutaka kubadilisha matokeo ya uchaguzi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu