Ziara ya Rais wa Afrika Kusini nchini yazaa matunda.

In Kitaifa

Ziara ya Rais wa Afrika kusini  nchini imezaa matunda mara baada ya kusainiwa kwa mikataba mitatu ya ushirikiano katika sekta mbalimbali, zitakazosaidia kukuza uchumi wa nchi hizo mbili.

Mikataba hiyo imesainiwa Ikulu jijini Dar es salaam wakati wa mkutano wa marais Dkt. John Magufuli na Rais Jacob Zuma.

Nchi hizo mbili zimesaini hati ya muhtasari wa makubaliano ya mkutano wa tume ya pamoja ya Marais kati ya Tanzania na Afrika Kusini, uliolenga kuboresha makubaliano yaliyofikiwa wakati wa mkutano huo.

Mikataba mingine ni hati ya makubaliano ya ushirikiano katika masuala ya Bio Anuwai kati ya Serikali ya Tanzania na Afrika Kusini, inayolenga kuboresha ushirikiano katika sekta ya wanyamapori na uhifadhi, na mkataba wa tatu ni hati ya makubaliano ya ushirikiano katika sekta ya uchukuzi, kati ya Serikali ya Tanzania na Afrika kusini uliolenga kuboresha sekta ya uchukuzi.

Hata hivyo, katika mkutano huo Rais Magufuli amesema ziara ya Rais Zuma imekwenda sambamba na mkutano wa kwanza wa tume ya Marais, ambapo umebainisha baadhi ya maeneo ya makubaliano.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu