Zimbabwe itajenga chuo kwa gharama ya dola bilioni moja

In Kimataifa

Zimbabwe itajenga chuo kwa gharama ya dola bilioni moja, kwa hemisha ya mtu anayelaumiwa kwa kuiongoza nchi kuelekea hali ngumu ya uchumi, Robert Mugabe.

Jonathan Moyo, ambaye ni waziri wa elimu aliwaambia waandishi wa habari kuwa wanachukua hatua hiyo kwa heshima ya rais huyo wa umri wa miaka 93, kwa wajibu wake katika elimu na uongozi mzuri.

Haijulikani pesa hizo zitatoka wapi kwenye nchi ambayo ukosefu wa ajira na umaskini ni tatizo kubwa.

Mwaka uliopita zaidi ya watu watu milioni moja nchini Zimbabwe walikumbwa na ukosefu wa chakula kotokana na ukame. Nchi hiyo wakati mmoja ilitajwa kuwa ghala la Afrika.

Licha ya hilo baraza la mawaziri limekubali kutumia dola milioni 800 kujenga chuo hicho kipya huko Mazowe, kilomita 35 nje ya mji wa Harare.

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu