Zomeazomea yasababisha COSATU kukatisha hotuba ya Rais Zuma katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi nchini Afrika Kusini

In Kimataifa

 Muungano wa vyama vya wafanyakzi nchini Afrika Kusini Cosatu umelazimika kukatisha ghafla hotuba za kuadhimisha siku ya wafanyakazi ikiwemo hotuba iliyokuwa ikitarajiwa kutolewa na Rais Jacob Zuma baada ya umati kuanza vurugu na baadhi yao kumzomea Zuma.

Rais huyo na ujumbe wake walionekana wakiondoka haraka kutoka kwenye jukwaa la maadhimisho hayo na kuchukuliwa na msafara mkubwa wa magari.

Cosatu ambao ni mshirika muhimu kisiasa wa chama tawala cha Afrika Kusini African National Congress ANC mwezi uliopita ulimtaka Zuma kujiuzulu baada ya kumuachisha kazi waziri wa fedha na kusababisha kushushwa kwa uwezo nchi hiyo kukopesheka.

Misururu ya maandamano imefanyika nchini humo kwa miezi kadhaa sasa kumshinikiza Zuma kuachia madaraka kutokana na kashfa za ufisadi na uongozi mbovu.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu