Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma anasema atafuatilia kwa karibu yale yanayoendelea katika taifa jirani la Zimbabwe.
Taarifa rasmi iliyotolewa na ofisi ya Bw. Zuma ililitaka jeshi kusuluhisha mzozo uliopo kwa njia ya amani.
Mwezi Agosti Afrika Kusini ilijipata kwenye mzozo wa familia ya Mugabe, wakati Grace Mugabe alidaiwa kumpiga mwamamitindo kwenye hoteli mjini Johannesbug
BI Mugabe hakushtakiwa baada ya serikali ya Bw. Zuma kumpa kinga.
